Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge zinafanyika leo mkoani Kagera ambapo TBC wanarusha matangazo hayo live.
Mkuu wa mkoa wa kagera fabian massawe anamalizia utambulisho ratina nyingine iendelee..kauli mbiu mwaka huu ni katiba mpya ni sheria kuu za nchi jitokeze kupiga kura. mgeni ni makam wa rais mohamed ghalib bilal.. Hivi sasa ni ujumbe kutoka znz ambao unawasilishwa na katibu mkuu wizara ya vijana utamaduni na michezo wa smz.
...........waziri wa utamaduni vijana na michezo fenelle mukangala anatoa hotuba ambapo anasema lengo kuu la mwenge ni kuwaunganisha watz, kuwamulika madhalim wanaoingalia tz kwa jicho la husuda na kusema kuwa, mbio hizi zitaendeleza mapambano dhidi ya madawa ya kulevya, rushwa na uhalifu wa aina mbalimbali...

.....wakimbiza mwenge wanaingia uwanjani sasa........haoooooooooo wako sita.....wanataka kuongoza ule wimbo maarufu wa sasa tunawasha mwenge.

mgeni rasmi makam wa rais mh. Ghalib Bilal anaendelea na hotuba, anaanza kwa kuwashukuru wana kagera kwa mapokezi mazuri waliyompatia. aidha anapongeza kagera kwa maandalizi mazuri waliyofanya. anawashukuru wageni toka nchi jirani hususan uganda na burundi kwa kuhudhuria sherehe hizi za uzinduzi.

anasema tz itaendelea kudumisha amani iliyopo hapa nchini ambayo tumeipokea toka kwa waasisi wa taifa hili. Anasema kukimbiza mwenge huu tunamuenzi mwalim julius nyerere ambaye ndio aliuasisi na alisema , tunauwasha mwenge huu juu ya mlima kilimanjaro umulike mipaka ya nchi yetu uwamulike maadui wa ndani na nje ya nchi, tunajikumbusha falsafa yetu ya upendo na amani kama taifa, tunadumisha tunu tulizoachiwa na waasisi wa taifa hili, lazima tupige vita kauli za kuligawa taifa, ujumbe wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu ni katiba ni sheria kuu ya nchi, jitokeze kupiga kura tupate katiba mpya.....pia kuna kauli zinazoambatana na kauli hii ambazo lengo lake ni kuhamasisha mapambano ya rushwa, madawa ya kulevya, haki za binadamu na uwajibikaji.

...........anaelezea mchakato wa kupata katiba mpya ambapo mh. rais aliridhia mchakato wa kuanza kwa mchakato mabadiliko ya katiba hapa nchini ambapo aliunda tume ya kupata katiba mpya na hivi sasa hatua iliyofikiwa ni majadiliano katika bunge la katiba lilioahirishwa mwezi uliopita. kazi hiyo bado inaendelea na ni imani yangu kubwa tutapata katiba yenye maslahi kwa wananchi.

anazungumzia mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria ambapo baada ya tafakuri kuu ya madhara ya gonjwa hili tumeona tuingize kama kauli mbiu katika mbio hizi.

..........anazungumzia mapambano dhidi ya gonjwa hatari la UKIMWI, ambapo 5% ya watz wenye umri juu ya miaka 19 wanaishi na virusi vya UKIMWI. kiwango cha maambuzi kiko juu (7% ) kwa mijini. ukimwi bado upo kwa kiwango kikubwa, tuchukue tahadhari.

kiwango cha ubaguzi na unyanyapaa kifikie sifuri

.........matumizi ya madawa ya kulevya
serikali kupitia tume ya kuthibiti madawa ya kulevya inapambana usiku na mchana kukomesha madawa ya kulevya kupitia vyombo vyake, jamii nzima inaombwa kutoa ushirikiano kuwaumbua wasambazaji na waagizaji

.......RUSHWA.....BADO VITENDO VYA RUSHWA vimeendelea kuwepo pamoja na mapambano mbalimbali ya serikali....tuikatae rushwa, tuseme hapana kwa rushwa....rushwa ni adui wa haki...
tumeadhimisha sherhe za mapinduzi hivi majuzi na wiki iliyopita tumeadhimisha sherehe za muungano wetu, tuzidi kuimarisha umoja wa taifa, tuepuke kauli za kuligawa taifa, tujikinge na maovu yote ili tz iweze kung'ara ndani na nje ya mipaka yetu.
Anawaasa wakimbiza mwenge kufanya kazi kwa ushirikiano, umoja na kwa nidhamu

';;;;;;;;;;sasa anaenda kuzindua rasmi mbio za mwenge, mwengeeeeeeeee eeeeeee mwenge mbio mbio mbio mwengeeeeeeeeeeeee eee mwenge mbio mbio mpaka makao makuuuuuuuuuuuuu mbio mbio mbioooooooooooooooooooooo

majina ya wakimbiza mwenge kitaifa 2014
1ibrahim mahamud kutoka mkoa wa mjini magharibi
2.yusuf athmani shesha kutoka dsm
3.jimai salum znz
4.wiston mbelwa kutoka mbeya
5.kiongozi wa mbio za mwenge ni dada DOTTO KASSANGA kutoka mkoa wa tabora mwenge unawashwaa sasa huooooooooooooooooooooooooo
............makam wa rais anamkabidhi mkimbiza mwenge wa uhuru ,mwaka huu DOTTO KASANGA, DOTTO anaomba dua na kuupokea mwenge huu
...................KISHA makam wa rais ataukabidhi mwenge huo kwa mkuu wa mkoa wa kagera, mkuu wa mkoa kagera anaomba dua ili mwenge ukimbie mkoani kwake kwa usalama na anataja thamani ya miradi itakayozinduliwa yenye thamani ya sh.milioni 15.

mwenge utazimwa na rais kikwete mkoani tabora tarehe 14 octoba mwaka huu

Quote By HarakatiNews View Post

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha Mwenge wa Uhuru wakati wa Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba Mkoa wa Kagera leo Mei 2, 2014. Mwenge huo unatarajia kuitimisha mbio zake Oktoba 14 mkoani Tabora, ambapo zinatarajia kufungwa na mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete.