Friday, June 20, 2014

Sunday, February 23, 2014

SKAUTI YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MINNE 2014-2017 NA KUMKUMBUKA MWANZILISHI WA CHAMA HICHO DUNIANI BADEN POWELL


Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hiyo, akikata utepe kuashiria kuzindua mpango mkakati wa Skauti wa miaka minne 2014-2017 Dar es Salaam jana. Kulia ni Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah na Makamu Mwenyekiti Skauti Taifa, Salim Mwaking'inda.
 Vijana wa Skauti wakiwa katika kambi ya mfano katika Maonesho hayo yaliyofanyika Uwanja wa Maonesho ya Biashara wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa.
 Vijana wa Skauti wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Kamishna Mtendaji wa Skauti, Brigedia General, Gerald Mkude (kushoto), akisaidia kufungua taarifa ya mpango mkakati wa miaka minne wa Skauti wa 2014-2017. Wengine kutoka kulia ni Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba na Makamu Mwenyekiti Skauti Taifa, Salim Mwaking'inda.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati), akionesha taarifa ya mpango mkakati wa miaka minne ya Skauti baada ya kuuzindua rasmi.
 Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah (kulia), akitoa nasaha zake kwa ufupi katika maadhimisho hayo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
 Vijana wa Skauti wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
 Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah (kulia),akimpatia nyenzo za kazi Elibariki Mmari kuwa Kamishna wa Mkoa wa Mwanza baada ya kumuapisha katika hafla hiyo. Baadhi ya Makamishna wa Mikoa na Manaibu wao walioteuliwa kushika nafasi hizo waliapishwa.
 Baadhi ya Makamishna walioteuliwa kuongoza katika mikoa mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (kushoto), akimpongeza Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mweka Hazina wa Shirikisho la Wabunge wa Skauti Duniani.
 Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan  Shah (kulia), akipeana mkono na Kamishna Mteule wa Mkoa wa Arusha, Shakir Badruddin baada ya kumuapisha katika sherehe hiyo.

Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati), akipata maelekezo katika kambi ya mfano ya skauti katika hafla hiyo.(Imeandaliwa na www.mwaibale.blogspot.com

No comments:

Post a Comment