Sunday, February 23, 2014
SKAUTI YAZINDUA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MINNE 2014-2017 NA KUMKUMBUKA MWANZILISHI WA CHAMA HICHO DUNIANI BADEN POWELL
![]() |
Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah. |
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati), ambaye alikuwa mgeni
rasmi katika sherehe hiyo, akikata utepe kuashiria kuzindua mpango
mkakati wa Skauti wa miaka minne 2014-2017 Dar es Salaam jana. Kulia ni
Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa
Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah na Makamu Mwenyekiti Skauti Taifa,
Salim Mwaking'inda.
Vijana wa Skauti wakiwa katika kambi
ya mfano katika Maonesho hayo yaliyofanyika Uwanja wa Maonesho ya
Biashara wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa.
Vijana wa Skauti wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
Kamishna Mtendaji wa Skauti,
Brigedia General, Gerald Mkude (kushoto), akisaidia kufungua taarifa ya
mpango mkakati wa miaka minne wa Skauti wa 2014-2017. Wengine kutoka
kulia ni Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni
Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah, Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba na Makamu
Mwenyekiti Skauti Taifa, Salim Mwaking'inda.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati), akionesha taarifa ya
mpango mkakati wa miaka minne ya Skauti baada ya kuuzindua rasmi.
Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti
Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah
(kulia), akitoa nasaha zake kwa ufupi katika maadhimisho hayo kabla ya
kumkaribisha mgeni rasmi.
Vijana wa Skauti wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti
Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah
(kulia),akimpatia nyenzo za kazi Elibariki Mmari kuwa Kamishna wa Mkoa
wa Mwanza baada ya kumuapisha katika hafla hiyo. Baadhi ya Makamishna wa
Mikoa na Manaibu wao walioteuliwa kushika nafasi hizo waliapishwa.
Baadhi ya Makamishna walioteuliwa kuongoza katika mikoa mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (kushoto), akimpongeza Kamishna
Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia,
Abdulkarim Esmail Hassan Shah kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya
Utendaji na Mweka Hazina wa Shirikisho la Wabunge wa Skauti Duniani.
Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti
Tanzania, ambaye pia ni Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Esmail Hassan Shah
(kulia), akipeana mkono na Kamishna Mteule wa Mkoa wa Arusha, Shakir
Badruddin baada ya kumuapisha katika sherehe hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Konsolata Mgimba (katikati),
akipata maelekezo katika kambi ya mfano ya skauti katika hafla
hiyo.(Imeandaliwa na www.mwaibale.blogspot.com
No comments:
Post a Comment