Tuesday, December 16, 2014

messager of peace

Chakula Cha Mchana Pamoja Na Watoto wa Mtaani.

Chama cha skauti Tanznaia kupitia wilaya ya ilala mkoani Dar Es Salaam  wameanziasha program ya kula chakula cha mchna pamoja na watoto wa mitaani kila wiki, kwa lengo la kuwavuta karibu ili kuwasadia kuondokana na maisha wanayo ishi sasa kwa kuwatafutia fursa mbalimbali zitakazo waendeleza kimaisha na hatimae waje kuwa wazazi bora katika familia zao. 


Vijana wa mitaani kutokea maeneo tofauti wakiwa katika picha ya pamoja na vijana wa skauti upanga makao makuu ya skauti. (Kamishna wa skauti (W) Ilala Bw. Crispin Criss Majia wakwanza kulia, akiwa na naibu wake Bw Piter Powel wapili kushot.)


Kamishna wa skauti (w) ilala akifanya mazungumzo na watoto wa mtaani na kuwafanyia usjili.


vijana wa mtaani wakisikiliza mongezi kutoka kwa kamishna wa wilaya ya ilala


Vijana wa skauti mkoa wa Dar es salaam wakibadilisahna mawazo na wageni wao (watoto wa mtaani)

Kamishna msaidizi wa wilaya ya ilala Bw. Peater Powel akiwanasihi vijana wa mitaani pamoja na vijana wa skauti juu ya athari za kujiweka katika makundi yasiyo faa.


Skaui wakiwahudumia chakula vijana wenzao washio mitaani kama tafrija ya kukutana kwao kila wiki.

Skaui wakiwahudumia chakula vijana wenzao washio mitaani kama tafrija ya kukutana kwao kila wiki.

Vijana wakiwa katika wakati eneo la skauti upanga (makao makuu ya skauti Tanzania) wakipata chakula cha mchana na skauti.

Vijana wakiwa katika wakati eneo la skauti upanga (makao makuu ya skauti Tanzania) wakipata chakula cha mchana na skauti
Kamishna wa skauti wilay ya Ilala mkoani Dar es salaam akiongea na vyombo vya habari kuhusiana na tukio zima la kuwakusanya vijana waishio mitaani na kuwaweka pamoja ili kusudi kuwasaidia waondokane na maisha waliyo nayo hivi sasa na kuwaanda kuwa raia wema na viongozi bora wa familia zao huko mbeleni.

Mmoja kati ya vijana waishio mtaani akiongea na vyombo vya habari juu yatukio hilo lililo wafanya wawe hapo katika eneo la skauti ikiwa ni pamoja na kuitaka serikali itoe msaada kwao na chama cha skauti kiujumla ili wafikie malengo waliyo ya kusudia kwao. Aidha kijana huyo alieleza juu ya changamoto zinazo wakabili ikiwa ni pamoja na mavazi, sitara(Pahali pa kulala), na chakula. Pia ameiomba serikali kuliangalia kwa makini suala lao na kupatiwa msaada ili waweze kufikia malengo yao waliyojiwekea katika maisha. 


Baada ya tukio zima kukamilika vijana wa skauti pamoja na vijana wa mitaani kwa pamoja walijumuika katika kuifurahia siku hiyo kwa kushiriki michezo mbali mbali ya kiskauti pamoja na kuimba kwa pamoja na kuleta udugu wa pamoja kama waishio katika familia moja.

Ilala District Local Scout Association
Have Lunch with Ilala Scout together with Street Children


Alhamisi, 3 Julai 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA AMANI DUNIANI. THEME ‘‘Right of Peoples to Peace”

SIKU YA KIMATAIFA YA AMANI DUNIANI

Siku ya Kimataifa ya Amani Duniani ni siku iliyopangwa na Umoja wa Mataifa kwa lengo la kukomesha vita, kutoa elimu juu ya amani na kuimarisha haki za binadamu ambayo husherehekewa tarehe 21 Septemba ya kila mwaka.

Mwaka huu 2014, Skauti (Tanzania) tutaungana na Mataifa mengine ya Dunia katika kusherehekea siku hii muhimu ikiwa imebeba kaulimbiu isemayo, ‘‘Right of Peoples to Peace” 

Lets meet to the summit of Mt. Kilimanjaro with the Peace message.

Mh. Abdulkarim Shah (Mb) Kamishna mkuu
 Chama Cha Skauti Tanzania.
Hivyo Ndugu, Skauti, kwa waraka huu tunaombwa kutangaza kauli mbiu hii kwa njia mbambali zitakazoweza kukuza Amani katika nchi yetu ya Tanzania na Dunia kwa ujumla.


                                                       
  







   Utaratibu wa Upandaji Mlima:



                                                                Umri:



> Skauti watakaoruhusiwa kupanda Mlima Kilimanjaro ni wale walio na umri wa miaka 12 na kuendelea, wavulana, wasichana na viongozi wao.

                                                                 Afya:

> Kila mshiriki atahitajika kupima afya yake katika kituo chochote cha afya kujihakikishia kuwa na afya bora kabla ya kupanda mlima.
                                       

                                                         Vifaa vya Kubeba


> Vifaa vya usafi:- Sabuni ya kuogea, sabuni ya kufulia, mswaki, dawa ya mswaki, mafuta ya mgando n.k.
> Mavazi:- Nguo nzito za baridi Masweta, jackets, nguo za michezo, soksi za mikono na miguu, kofia za baridi n.k.

                                                           Ada ya Ushiriki:


> Kila mshiriki atawajibika kuchangia kiasi cha Tshs. 150,000/=  ambayo itajumuisha gharama za kuingia mlimani, gharama za kupanda mlima, chakula na malazi kwa kipindi chote cha siku za kupanda mlima.
> Gharama nyingine za usafiri kutoka na kurudi katika mikoa husika na ada za kutoka nje ya mikoa zitagharamiwa na mshiriki mwenyewe binafsi.
> Malipo ya kila mshiriki yanahitajika kulipwa kupitia Akaunti ya Chama cha Skauti Tanzania, iliyoko katika Benki ya National Bank of Commerce (NBC) tawi la Samora,
Account Number 012103010625. Baada ya malipo, Makamishna wa Mikoa watawajibika kutuma majina ya Skauti watakaolipa na namba za stakabadhi za malipo ya Bank Makao Makuu ya Chama kwa uthibitisho.
                                                         

                                                            Kuthibitisha Ushiriki:

> Washiriki watahitajika kuthibitisha ushiriki wa kupanda Mlima kwa Kujaza fomu na kuirejesha Makao Makuu ya Chama cha Skauti Tanzania kwa njia ya barua pepe (Email) kabla ya tarehe 18 Julai 2014 au kupitia kwa Makamishna wa Mikoa.

                                                                     RATIBA:


S/No.          TAREHE                                   TUKIO                                       MUHUSIKA                 
1.          16 - 17 Septemba 2014        Kuwasili Mkoani Kilimanjaro    Uongozi wa Skauti Mkoa wa
                                                                                                                Kilimanjaro na Uongozi wa                                                                                                            Skauti\ Makao Makuu.
                                                                                                                                                                
  2.        18 - 21 Septemba 2014        Kuwasili Kileleni mwa Mlima           Skauti wapanda Mlima
                                                           Kilimanjaro                                                                       
  3.        22 Septemba 2014                Kurejea chini ya mlima Skauti         wapanda Mlima              
  4.        23 Septemba 2014                Kuondoka Kilimanjaro                   Skauti wote                     

Ni mategemeo yetu kuwa Skauti tutajitokeza kwa wingi kuonyesha mshikamano wetu katika kupeleka ujumbe wa Amani kwa njia kupanda mlima wetu Kilimanjaro, Mlima mrefu Barani Afrika wenye kuleta Amani, Upendo na Matumaini pale ambapo hakuna matumaini

Kwa maelezo zaidi kuhusu upandaji mlima, na watakao hitaji fomu za ushiriki {kwenda kusherekea siku ya Amani duniani} tafadhali tutumie ombi hilo la kupata fomu hiyo kupitia :

Mobile: +255 713 295 715
Tell: +255 2222 153342
Fax: +255 2222 1248 807
Email: Tanzani Scout Association


MLIMA KILIMANJARO








Alhajj. Omar Khatib Mavura Mratibu Messengers
of Peace Taifa.



















Murtadhwa Rashid Abdallah Mratibu Messengers
of Peace Mkoa (Dar-es-salaam)



















https://www.facebook.com/pages/Messengers-of-Peace-Tanzania-MOPTZ/1408726232704353?ref_type=bookmark

HATIMAE JUKWAA LA VIJANA LAPATA WAJUMBE WA KAMTI KUU TANZANIA. {TANZANIA YOUTH COMMITTEE} 2014-2016

JUKWAA LA VIJANA TANZANIA, {TANZANIA YOUTH FORUM} 28-30 JUNE,2013 BAHATI CAMP-MOROGORO.


          Chama cha Skauti Tanzania chapata uongozi mpya wa jukwaa la vijana "Youth Forum" yenye wajumbe sita (6) chini ya mwenyekiti Bw. Chacha N. Mwita ambae amekabithiwa rasmi jukumu hilo mapema wiki hii baada ya kuchaguliwa na na vijana walioshiriki jukwaa hilo kutoka mikoa tofauti iliyopo nchini Tanzania, uchaguzi huo uliofanyika 28-30 june, 2014 sambamba na kuendeshwa kwa kongamano hilo juu ya maendeleo ya uskauti na vijana wa skauti kiujumla.


Timu iliyoshiriki jukwaa la vijana 


        















         

         Aidha nae Bw. Chacha (baada ya kuchaguliwa kwa nafasi hiyo) aliitaka kamati yake kuwa makini na kuwa tayari kukitumikia chama cha Skauti Tanzania (kwa kutumia nyadhifa walizo nazo kama viongozi wa vijana nchini) kwa hali na mali ili kuhakikisha wanafikia malengo na dhamira ya chama cha Skauti kidunia.
         Pia Bw. Chacha (Mwenyekiti) alitoa wito kwa vijana wa skauti nchini (Tanzania) kuonesha na kuwapa ushirikiano wanakamti hiyo ya jukwaa la vijana la Tanzania iliyoundwa 30 june, 2014  ili kufanikisha utendaji wa kamati hiyo.

       
         Vile vile Ndugu. Murtadhwa R. Abdallah (katibu mkuu wa jukwaa la vijana nchini, pia ni mratibu wa wajumbe wa amani) alisisitiza juu ya ushirikiano wa vijana (skauti) na kamati hiyo ili kuleta manufaa kwa wana chama (skauti) katika nche yetu na ulimwengu kiujumla. 
          Ndugu katibu mkuu wa jukwaa la vijana nchini, pia ni mratibu wa wajumbe wa amani Bw. Murtadhwa R. Abdallah aliwaeleza kwa upana zaidi wajumbe walio hudhuria kongamano hilo juu ya masuala ya ujumbe na wajumbe wa amani (Semina fupi elekezi) na kuwataka wajumbe hao waliohudhuria kongamano hilo kuwa wajumbe (mabalozi) wa kulifikisha na kulifanyia kazi suala la ujumbe na wajumbe wa amani katika mikoa yao na kuanza kulifanyia kazi kwa vitendo suala hilo.
Ndugu. Murtadhwa R. Abdallah (katibu mkuu wa jukwaa la vijana nchini, pia ni mratibu wa wajumbe wa amani)
Sambamba na viongozi hao wa jukwaa la vijana, pia Kamishna mkuu msaidizi Mwl. Merry Anyitike (msimamizi wa programu za vijana nchini) aliipa baraka kamati hiyo ya jukwaa la vijana nchini na kuwapa wosia wa kuwa waadilifu na kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kufuata misingi na kanuni za skauti. 
Kamishna mkuu msaidizi Mwl. Merry Anyitike (msimamizi wa programu za vijana nchini)

        Pia alimalizia kwa kusema kuwa "Jukwaa la vijana ni moja ya chombo kinacho tumiwa katika kufanikisha shughuli za chama, hivyo ni vyema vijana kukitumia chombo hicho katika kuleta mafanikio ndani ya chama..



Vijana wa skaut wakiwa katika kongamano mkoani Morogoro.

Vijana wa skaut wakiwa katika kongamano mkoani Morogoro.

Vijana wa skaut wakiwa katika kongamano mkoani Morogoro.

Kamishna mkuu msaidizi Mwl. Merry Anyitike (msimamizi wa programu za vijana nchini)akitoa somo kwa vijana waliohudhuria jukwaa hilo.



UONGOZI WA KAMATI YA JUKWAA LA VIJANA TANZANIA 2014-2016




Ndugu, CHACHA MWITA 
(Korogwe)
MWENYEKITI

Bi, ANNA EMMANUEL 
(Dodoma)
NAIBU MWENYEKITI
Ndugu, MURTADHWA RASHID
 (Dar Es Salaam)
KATIBU








Ndugu,TITO JACKSON
(DarEs Salaam)
MJUMBE
Ndugu, ALLEN MPANDE
 (Morogor)
MJUMBE
Ndugu, ELAM MOSSES
 (Mbeya )

MTUNZA HAZINA

Jumamosi, 17 Mei 2014

MESSENGERS OF PEACE.

WAJUMBE WA AMANI {MESSENGERS OF PEACE}

Nimradi ulioundwa na kamati na kamati kuu ya skauti ya dunia kwa kukuza na kuitambua miradi na huduma zinazochangia  amani duniani.
   *LENGO LA MESSENGERS  OF PEACE
  - Kuhamasisha mamilioni ya vijana wa kike na wakiume kwa ajili ya dunia kufanya kazi kwa ukaribu na hata kufikia amani.
*NJIA YA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA
   -Sanaa
   -Vyombo vya habari
   -Mitandao ya kijamii
   -Mpango wa skauti kutoka makao makuu [wosm] ni kushirikiana na vijana duniani kote juu ya wanayo yafanya na kuhamasisha skauti wenzao dhidi ya kuchukua jitihada hizo katika jamii zao.
   *WAENDESHAJI WA MPANGO  WA [MOP]
    -Mpango mradi huu unaendeshwa na kamati kuu ya skauti duniani [wosm]
    -Unasimamiwa na taasisi ya skauti ya dunia pamoja na ..........
    -Unatekelezwa na vijana wa kujitolea duniani kote.
    *JINSI GANI MRADI HUU UNAVYOENDELEA
     -Mpango huu wa [mop] umetokana na miaka 10 iliyopita katika mpango wa "gift of peace" ambao uliongoza [kushiriki nafasi ] kwa zaidi ya skauti millioni 10 katika nchi 110 kwa kufanya kazi ya amani katika jamii [mfano qiblatayn scout group walipata tuzo]
    -Mfalme Abdallah [saudi] alibainisha kuwa ni wajumbe wa amani kutokana na mradi huo"Gift of peace"
    -Mwenyekiti wa kamati ya kusimamia skauti duniani aliweka rasmi [Skauti kuwa wajumbe wa amani] sep,2011.
    *WADHAMINI WA MRADI
    -[WOSM] kama sehemu ya wajumbe wa amani, ofisi ya skauti ya dunia ina mfuko maalum wa kuendesha miradi hiyo duniani kote, kwa mashirika ya skauti katika nchi husika.
     *NAFASI YA KUUNGANA NASKAUTI WENGINE
      - Unaweza kuweka kupitia miradi waliyofanya skauti wengine duniani kwa kupitia www.scoutmessengers.com

Jumanne, 4 Februari 2014

SKAUTI WATOA MSAADA WA HUDUMA KATIKA MAAFA YA MAFURIKO MJINI MOROGORO-DUMILA.

SKAUTI WATOA MSAADA WA HUDUMA KATIKA MAAFA YA MAFURIKO MJINI MOROGORO-DUMILA.


Skauiti washiriki katika kutoa msaada katika maafa ya mafuriko yaliyo tokea mjini morogoro-dumila dhidi ya mvua zilizo nyesha kwa wingi hadi kupelekea mafuriko wilayani humo{dumila}. kufuatia maafa hayo chama cha skauti tanzania kupitia kamishna msaidizi kitengo cha maafa kilipeleka kikosi cha huduma na uokoaji majini na nchikavu ili kushirikiana na vikosi vyengine vya serikali na binafsi katika kutoa msaada unaohitajika.
Kamishna mkuu msaidizi kitengo cha maafa. Alhajj, Juma Massud
Kufuatia tukio hilo skauti pia iliweza kuzaa matunda juu ya jambo kubwa wlilolifanya katika kambi ya dhalura iliyo tengenezwa kufuatia tukio hilo, serikali kupitia mkuu wa mkoa wa morogoro iliikabidhi skauti dhamana ya kuandaa na kuweka maingira ya kambi kwakuwa skauti ni wazoefu juu ya masuala ya kambi.
Skauti wakiwa katika shughuli za ujenzi wa vyoo kwaajili ya kukamilisha zoezi la uaandaji wa eneo la kambi kama walivyo agizwa na mkuu wa mkoa wa morogoro.
Skauti wakiwa katika shughuli za ujenzi wa vyoo kwaajili ya kukamilisha zoezi la uaandaji wa eneo la kambi kama walivyo agizwa na mkuu wa mkoa wa morogoro.
Lakini pia kama Skauti walichukua nafasi hiyo kwa kukitan
gaza chama cha Skauti katika jamii na kusambaza ujumbe wa Amani kupitia vijana wa shule ya sekondari Dumila na wana kijiji kiujumla. pia waliweza kuanzisha kundi la skauti na kulipa mafunzo ya mwongozo kwa kuanzia juu ya skauti na shughuli zake kiujumla.
 Ni wanachama wapya wa skauti ambao walikubali kwa moyo wa dhati kujiunga na chama cha skauti baada ya kuona yale waliofanya skauti katika kusaidia kijiji chao baada ya mafuriko kutokea.
 Vijana wadogo wakiwa pamoja na skauti katika kuashiria upendo wa dhati juu ya walio watendea baada ya maafa yalio wakuta katika kijiji chao-dumila.
 Wana kijiji wakiwa katika picha ya pamoja na skauti baada ya kuwahubiria uskauti na madhumuni yake na kuwaachia ujumbe wa Amani ili waweze kuishi vyema kwa kufuata misingi halisi ya kibinaadamu.
Kiongozi wa kikosi chahuduma na uokoaji{majini} akiwa katika kiashirio cha Ujumbe wa Amani baada ya kuzungumza na wakaazi wa kijiji cha Dumila mjini Morogoro.
Kiongozi wa kikosi cha maafa na uokoaji{majini}, pia ni msimamizi wa vijana katika masuala ya Ujumbe Amani Tanzania {katika ngazi ndogo ya Taifa} akiwa na mmoja kati ya vijana wa kijiji hicho kilicho kumbwa na maafa ya mafuriko.
Mwisho kiongozi huyo aliwataka skauti wote kuwa naa ushirikiano wa pamoja katika kukijenga chama cha skauti katika misingi na maadili yaliyo mema, na kuwa tayari akati wowote kulitumikia taifa pale inapotokea tatizo kama hilo la mafuriko na mengineyo. pia alisisitiza juu ya kundi hilo jipya la skauti kuwa na moyo wa upendo kwa kila mmoja na kpeana ushirikiano na kuishi kutokana na misingi, kanuni na ahadi ya skauti.

Jumatano, 8 Januari 2014

 vijana wa skauti kanda ya afrika mashariki wakijadili kuhusu masuala ya vijana katika mkutano kuu wa nane wa kanda hiyo ya Afrika Mashariki huku kaulimbiu ikisema (scout promoting peace and good citizen ship).
 waongoza mada wakisikiliza hoja kutoka kwa wajumbe wa wa mkutano huo.(kutokea kulia ni Malik kutoka Tanzani, anaefata ni Benta kutokea Kenya, anefata ni Brian kutokea uganda na wamwisho ni prience kutokea Burundi)
 Baadhi ya wajumbe wa mkutano huowa nane wa kanda ya Afrika mashariki kutokea kulia ni Murtadhwa (Tanzania), Anita (Uganda), Anna(Tanzania) na Khalid (Uganda).
moja ya waongoza mada (Malik) wa kutokea Tanzania alikua akizungumzi juu ya kaulimbiu ya mkutano huo isemayo "skauti kutangaza Amani na kuwafanya raia kuwa wema