pamoja na mjadala mzito kuhusu muundo wa serikali mbili au
tatu,lazima tudumishe muungano tulioachiwa na waasisi wetu, pia
wanasiasa muache kufua majina ya waasisi wetu kwa maslahi yenu ya kutaka
kujionesha kwa watanzania, sisi watanzania tunawaheshimu sana waasisi
wetu na tumechukia sana kudhalilishwa kwao na watanzania wenzetu hasa
wanaotuwakilisha kwa mambo makubwa ya kimataifa, hamuoni hata mataifa
mengine wanawaenzi hawa waasisi wetu? chukua mfano siku ya mazishi ya
marehemu Tata Madiba (Mandela) jina la baba wa taifa letu lilikuwa
likitajwa na kuheshimiwa, je ninyi kwanini mmetugeuka? Wanasiasa na
vyama venu mjiangalie na mjitathimini kama watanzania wanawakubali kwa
matendo yenu mabaya kwa wataifa.
No comments:
Post a Comment