MWENGE WA UHURU 2014 WAMALIZA MBIO ZAKE MKOANI RUKWA LEO, WAMMULIKA MLEMAVU WA NGOZI (ALBINO) ALIYEKATWA MKONO MWAKA JANA
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (katikati) akishiriki mbio za Mwenge wa Uhuru (2014) na viongozi wa mbio hizo kitaifa, viongozi na wafanyakazi wa Serikali, vyama vya siasa Mkoani Rukwa na wananchi muda mfupi kabla ya kukabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro baada ya Mwenge huo kukamilisha mbio zake Mkoani Rukwa leo tarehe 25-05-2014. Mwenge huo wa Uhuru mkoani Rukwa ulitembelea miradi ya maendeleo 28 na vikundi 27 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni nne (4).
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjCckVLYQS8z1z2vUXzTBad4Hxdkkb4bMAwLWh_oOTNXqdRSpBZxRFI-cDxel0yfC_ZrLKkjjxMs_S0YtTtnr46oEkAX20Hp-uk9N3kJeNb_syFzJbJTo2W3wDTi9__UOQKgeh4jLbmKg8l/s1600/PIC+6.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6K8DoMYfPNRvd9I0WT9LHaIdxIIMi3LXMPBfIA40j0wC_lgEBnuSdDwOEl4kRpdsGRUhsqeZUxxW4kHtsK-CQQt1YgNZC9eKKeOUP2mZNpKGcxxIYcVUbi0EE09bvrMsFr9m8gKz0wv5y/s1600/PIC+3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJs4fDsDnemgRRJS41NcArnE0N3dUlbyOdCnNztNLG_7mfPzl_BPOSINY4HV7381bP0xbP5B4p2pmUXZhrqMVrEP5h4AUmaKWg5hyphenhyphenrd6iPkIFNo15LcN6EF4CZWju6tuhhMuwBY5BuQ1Gb/s1600/IMG_1859.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijZxIa-3APD5hUVf8ZbLNuxxtmeiThCjnyWdza-5ucbRMHRwLg2_z1KY_z7v1LS6bhjrvv6zhh1N2pzqlPIZN5rV5PYBqpQ7U_cAMXuM96Z3Edqaodpf9D3K1PrHWK7DqUU6ftPZS_WYUh/s1600/PIC+4.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjEuzfXF6hoEs3MaJoydNeSOJhuroz3WLkNDRPNyt3jlx68VJYJQp2WSIFsmOeu23U26YsmdVcHJkTAmZX0ag95m_lpWHQH4iDFoyntii6OMOg5-GoXt1Ys9dWqRJQAqX5UlFc5i9TWy8TL/s1600/PIC+5.jpg)
Mlemavu wa ngozi
Bi. Maria Chambanenge mkazi wa Sumbawanga ambaye alisababishiwa ulemavu
mwingine wa viungo mwaka jana 2013 na watu wasiojulikana baada ya kukatwa mkono
wake wa kushoto kwa imani za kishirikina akishika Mwenge wa Uhuru jana tarehe
24-05-2014 ulipotembelea kijijini kwao kuzindua mradi wa maji na kumkabidhi
msaada wa ng'ombe wawili wa kulimia aina ya Maksai (hawapo pichani) na jembe la
kulimia wanyama (Plau) vikiwa na thamani ya Tsh. Milioni 2.3 kama msaada wa
kujikimu kutoka kwa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa mama huyo.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)
No comments:
Post a Comment