SHEREHE ZA KUMBUKUMBU YA KUZALIWA BADEN-POWELL ZAFANA
MAKAMISHNA WA SKAUTI MIKOA NA NAIBU WAO WAAPISHWA
Sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwasisi wa Skauti Duniani Marehemu Baden-Powell zimefanyika katika nchi mbalimbali za Dunia.
Katika Jiji la Dar Es Salaam Sherehe hizo zilifanyika katika Kiwanja cha Kimataifa cha Biashara cha Mwalim Julius Kambarage Nyerere (Saba-Saba) barabara ya kilwa.
Shughuli hiyo iliyoandaliwa na Skauti Mkoa wa Dar Es Salaam kwa kamati iliyoongozwa na Kamishna wa Skauti wa Mkoa huo Ndugu Abubakar Mtitu.
Katika sherehe hiyo, Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania (TSA) ndugu Abdulkarim Ismail Shah aliwaapisha Kamishna wa Mikoa na Manaibu wake.
Pia katika sherehe hiyo chama cha Skauti Tanzania kilizindua Mpango Mkakati wa Chama hicho.
Mgeni wa rasmi katika Sherehe hiyo alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Ufundi Stadi Bi. Consolata Mgimba kwa niaba ya Rais wa Chama ambaye ni Waziri wa Elimu na Mafunzo Mheshimiwa Shukuru Kawambwa alifika katika eneo la sherehe mnamo saa nne asubuhi tayari kwa kupokea maanamano na kuaza kwa sherehe hiyo.
![]() |
Mgeni rasmi Bi. Consolata Mgimba Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Ufundi akivishwa Skafu na Skauti tayari kupokea maandamano ya Skauti, tarehe 22 Februari 2014 |
![]() |
Mgeni rasmi Bi. Consolata Mgimba Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Ufundi akitoa salamu kwa niaba ya Rais wa Chama ambaye ni Waziri wa Elimu na Mafunzo Mheshimiwa Shukuru Kawambwa |
Wednesday, February 19, 2014
RATIBA YA SHEREHE YA SIKU YA MWANZILISHI WA SKAUTI DUNIANI LORD BADEN POWEL - 22 FEBRUARI 2014
MUDA
|
TUKIO
|
MHUSIKA
|
Saa 3:00 Asubuhi
|
Skauti kuwasili Uwanja wa Taifa
|
Skauti wote
|
Saa 3:30 Asubuhi
|
Maandamano kuelekea viwanja vya Mwl. Nyerere, Saba Saba
|
Skauti na Viongozi wao
|
Saa 3:30 Asubuhi
|
Ø Viongozi wa Chama kuwasili Ukumbini.
Ø Skauti Mkuu na Mwenyekiti Kamati Tendaji(T) kuwasili ukumbini.
Ø Wageni waalikwa kuwasili ukumbini.
|
Kamati ya Mapokezi/ MC
|
Saa 4:00 Asubuhi
|
Mgeni Rasmi kuwasili Uwanjani na kuvishwa Skafu.
Ø Mgeni Rasmi kupokea maandamano.
|
Kamishna Mkuu,
Naibu Kamishna Mkuu,
Kamishna wa Mkoa(DSM)
Kamishna Mtendaji,
|
Saa 4:05
Asubuhi
|
Mgeni Rasmi kuingia Ukumbini.
Ø Wimbo maalum (Twamkumbuka Mzee wetu Baden Powell)
Ø Utambulisho wa wageni maalum
|
Skauti wote
Kamishna Mkuu
|
Saa 4:15
Asubuhi
|
Nasaha za Skauti Mkuu
|
Skauti Mkuu
|
Saa 4:30 Asubuhi
|
Burudani
|
MC
|
Saa 4:40 Asubuhi
|
Uzinduzi wa Mpango Mkakati
(Strategic Plan 2014 – 2017)
|
Mgeni Rasmi,
Kamishna Mkuu Msaidizi Miradi.
|
Saa 4:50 Asubuhi
|
Kuapishwa kwa Makamishna wa Mikoa
Ø Burudani.
|
Kamishna Mkuu
Skauti.
|
Saa 5:20 Asubuhi
|
Kuwekwa saini kwa Mkataba wa Hifadhi ya Msitu wa Vikindu
|
Kamishna Mkuu
Mkurugenzi wa Hifadhi ya Misitu
|
Saa 5:30 Asubuhi
|
Burudani (Maonesho ya Sanaa ya mapigano)
|
Kikosi cha Rova
|
Saa 5:40 Asubuhi
|
Tukio maalum
|
MC
|
Saa 5:50 Asubuhi
|
Nasaha za Mgeni Rasmi
|
Mgeni Rasmi
|
Saa 6:00 Mchana
|
Kurudia Ahadi
|
Wote/ Kamishna Mkoa
|
Saa 6:05 Mchana
|
Neno la shukrani
|
Mwenyekiti Kamati Tendaji
|
Saa 6:15 Mchana
|
Chakula
|
Kamati ya Chakula
|
MWISHO
|
No comments:
Post a Comment